
Mkurugenzi mtendaji wa kituo cha mafunzo ya ujasiriamali Tanzania, kanda ya Zanzibar bibi Lucy Mwaipopo akitoa maelezo mbele ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad kuhusiana na bidhaa mbali mbali za wajasiriamali wa mradi wa MKUAJI. Wa pili kushoto ni Mwakilishi wa Jimbo la Mtoni, Nassor Ahmed Mazrui
Mradi wa Kuendeleza Ujasiriamali na Ajira (MKUAJI), ni mradi wa wajasiriamali ulioanzishwa katika jimbo la Mtoni Wilaya ya Magharibi Unguja hivi karibuni. Wazo la kuanzishwa kwa mradi huo lilitokana na Mwakilishi wa Jimbo hilo la Mtoni Mhe. Nassor Ahmed Mazrui ambaye pia ni Waziri wa Biashara, Viwanda na Masoko Zanzibar. Continue Reading


